#KILA ULIMI, ni wimbo wa Nne katika IBADA YA MOYO WA SHUKRANI iliyofanyika 10 NOV, 2023 katika kanisa la AICT Chang’ombe, Sokota Temeke Dar es salaam.

Ndani ya wimbo huu AIC Chang’ombe Choir tunamshukuru Mungu kwa baraka zake alizotukirimia kwa zaidi ya miaka 35 tangu kuanzishwa kwa kwaya yetu. Tunaamini wimbo huu utaenda kufanyika Baraka katika maisha yako. MUNGU AKUBARIKI.

Lyrics

Iweni na nia iyo, hiyo
ndani yenu
ambayo (ambayo)
Ilikuwemo pia ndani ya Kristo Yesu ( Kristo Yesu)

Ambaye (ambaye)
Yeye mwanzo (Yeye mwanzo)
Alikuwa Yu na namna ya MUNGU

Naye hakuona
kule kuwa sawa na MUNGU
Kuwa ni kitu
Cha kushikamana nacho

Bali alijifanya
kuwa hana utukufu
Akatwaa namna ya mtumwa
Akawa mfano wa mwanadamu (wa mwanadamu)
huyu YESU (huyu YESU)

Tena alipo onekana
Ana mwili kama mwanadamu
Alijinyenyekeza
Akawa mtii
Hata mauti na mauti ya Msalaba
(Mauti ya Msalaba)

Kwa hiyo tena MUNGU
Alimwadhimisha mno
Akamkirimia jina
Lile lipitalo kila jina
Ili kwa jina la YESU
Kila goti lipigwe
Na kila ulimi ukiri

Na kila ulimi ukiri
Ya kuwa YESU Kristo
Ni Bwana
Kwa utukufu wa MUNGU Baba
Utukufu wa MUNGU Baba

Video

AIC Chang’ombe Choir (CVC) ft. Zoravo – KILA ULIMI (Official Live Video)

Shares:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *