This song is a prayer inspired by Psalm 139:7-12, Ezekiel 47:3-5 and Phil 3:12 May grow to know God in a deeper way.

Lyrics

Verse 1:
Ni pahali gani pa kukimbia uwepo Wako eh?
Nauliza ni wapi pa kujificha uso Wako Yahweh?
Nikipanda mbingu (Wewe Upo)
Nikishuka kuzimu (bado Upo)
Nikijivika giza (We Waona)
Hakuna mahali popote (We Haupo)
Nataka nikujue unijuavyo
Natamani nishike lile ambalo kwa ajili Yako nimeshikwa

Chorus:
Nataka nizame, nizame, nizame
Kwa uwepo wako nizame, nizame
Naomba Unifunike kwa Mbawa Zako
Na tena Unijaze na Roho Wako
Aaaah nizame
Aaaah nizame

Verse 2:
Fikira Zako Baba (zina thamani kwangu)
Maneno Yako Baba (yana thamani kwangu)
Chunguza moyo wangu ili (Ujue mawazo yangu)
Kagua njia zangu uniongoze (kwa njia za milele)
Nikufahamu Unavyo nifahamu
Natamani nishike lile ambalo kwa ajili Yako nimeshikwa

Chorus:
Nataka nizame, nizame, nizame
Kwa uwepo wako nizame, nizame
Naomba Unifunike kwa Mbawa Zako
Na tena Unijaze na Roho Wako
Aaaah nizame
Aaaah nizame

Video

Alice Kimanzi – Nizame |Official Video|

Shares:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *